Psalms 77:1-6
Matendo Makuu Ya Mungu Yanakumbukwa
(Kwa Mwimbishaji: Mtindo Wa Yeduthuni. Zaburi Ya Asafu)
1 aNilimlilia Mungu ili anisaidie,
nilimlilia Mungu ili anisikie.
2 bNilipokuwa katika taabu, nilimtafuta Bwana,
usiku nilinyoosha mikono bila kuchoka
na nafsi yangu ilikataa kufarijika.
3 cEe Mungu, nilikukumbuka wewe, nikalia kwa huzuni;
nikatafakari, roho yangu ikadhoofika.
4 dUlizuia macho yangu kufumba;
nilikuwa nasumbuka, nikashindwa kusema.
5 eNilitafakari juu ya siku zilizopita,
miaka mingi iliyopita,
6 nilikumbuka nilivyoimba nyimbo usiku.
Moyo wangu ulitafakari
na roho yangu ikauliza:
Copyright information for
SwhKC