Psalms 77:1-6

Matendo Makuu Ya Mungu Yanakumbukwa

(Kwa Mwimbishaji: Mtindo Wa Yeduthuni. Zaburi Ya Asafu)


1 aNilimlilia Mungu ili anisaidie,
nilimlilia Mungu ili anisikie.

2 bNilipokuwa katika taabu, nilimtafuta Bwana,
usiku nilinyoosha mikono bila kuchoka
na nafsi yangu ilikataa kufarijika.


3 cEe Mungu, nilikukumbuka wewe, nikalia kwa huzuni;
nikatafakari, roho yangu ikadhoofika.

4 dUlizuia macho yangu kufumba;
nilikuwa nasumbuka, nikashindwa kusema.

5 eNilitafakari juu ya siku zilizopita,
miaka mingi iliyopita,

6 nilikumbuka nilivyoimba nyimbo usiku.
Moyo wangu ulitafakari
na roho yangu ikauliza:

Copyright information for SwhKC